1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi Ukraine limeshambulia uwanja wa ndege Urusi

18 Aprili 2024

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema jeshi lake limeshambulia uwanja wa ndege mkubwa wa Urusi wa Dzhankoi katika eneo linalokaliwa la Crimea na kuwasifu makamanda wake walioongoza oparesheni hiyo.

https://p.dw.com/p/4eu0U
Kyiv, Ukraine | Rais Volodymyr Zelensky
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskyPicha: Ukrainian Presidency/abaca/picture alliance

Zelensky ametaja oparesheni hiyo kuwa ni yenye mafanikio kutokana na jeshi la Ukraine, kuripoti kuharibu miundombinu pamoja na vifaa vya kijeshi vya Urusi katika oparesheni hiyo iliofanyika kaskazini mwa rasi ya Crimea iliyonyakuliwa na kukaliwa na Urusi mwaka 2014.

Soma pia:Zelensky atoa wito wa mshikamano baada ya shambulio la Urusi

Kwa upande mwingine Urusi imeendelea kuvurumisha makombora katika miji ya Ukraine, ambapo makombora matatu yameanguka katika mji wa kihistoria wa Chernigiv na kuuwa watu 17.

Serikali ya Kyiv imeendelea kuomba mifumo ya ulinzi wa anga kutoka kwa washirika wake, ikiwemo Ulaya na Marekani.