1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yataka msaada wa silaha kwa Sudan usitishwe

30 Aprili 2024

Marekani imetaka msaada wa silaha kwa pande zinazohasimiana nchini Sudan kusitishwa, huku ikionya kwamba historia katika eneo la Darfur ambako kulishuhudiwa mauaji ya halaiki miaka 20 iliyopita "inajirudia."

https://p.dw.com/p/4fLbB
Sudan | Abdel Fattah Abdelrahman al-Burhan na Mohamed Hamdan Dagalo
Mahasimu wanaowania madaraka Sudan, Jenerali Abdel Fattah Abdelrahman al-Burhan (kulia) na Mohamed Hamdan Dagalo.Picha: Mahmoud Hjaj/AA/picture alliance

Balozi wa Marekani Umoja wa Mataifa, Linda Thomas-Greenfield, aliyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kuongeza kwamba El Fasher mji mkuu pekee katika jimbo la Darfur ambao haujashikiliwa na vikosi vya kijeshi uko "kwenye ukingo wa mauaji makubwa."

Thomas-Greenfield ameongeza kwamba kuna ripoti za kuaminika kwamba vikosi vya RSF pamoja na washirika wake wameteketeza vijiji kadhaa magharibi mwa El Fasher na kuna mpango wa mashambulizi karibu na mji huo.

Soma zaidi: Nani anawaunga mkono makamanda wanaoipigania mamalaka Sudan?

Sudan ilitumbukia katika mzozo mnamo Aprili 2023 kufuatia mvutano baina ya majenerali wawili, Abdel Fattah Burhan anayeongoza vikosi vya serikali  na Mohammed Hamdan Dagalo anayeongoza wanamgambo wa RSF.

Mzozo huo umesababisha maelfu ya watu kuuwawa na wengine mamilioni kukimbia makaazi yao.