1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 10 wajeruhiwa katika mashambulizi kusini mwa Syria

Ibrahim Swaibu1 Mei 2020

Wizara ya ulinzi ya Syria iilitangaza kuwa mashambulizi hayo yaliotokea Mei mosi yalilenga ghala la silaha za jeshi katika kambi inayopatikana kwenye jimbo la Homs katikati mwa Syria

https://p.dw.com/p/3bfMm
Türkisches Militär in Syrien - 27. Feb. 2020
Picha: Getty Images/A. Tammawi

Zaidi ya watu kumi wamejeruhiwa  nchini Syria baada ya mashambulizi kwenye ghala la silaha za jeshi katika jimbo la Homs lilioko katikati mwa nchi hiyo, wizara ya ulinzi ya Syria imetanganza. Mashambulizi hayo yanadaiwa kutekezwa na Israel ikilenga kundi la Hezbollah na vikosi vya Rais Bashar Assad.

Televisheni ya taifa nchini Syria mapema imetanganza kutofahamu sababu ya mashambulizi hayo, lakini shirika la kutetea haki za binadamu la Syria lenye makao yake Uingereza limesema mashambulizi hayo yalifanywa na Israel ikitumia makombora kulilenga ghala la zana za kijeshi la kundi la Hezbollah katika kambi ya Ibn a-Haitham.

Mkuu wa shirika hilo, Rami Abdel-Rahman, ameviambia vyombo vya habari vya Syria kuwa zaidi ya raia 10 wa kawaida wamekimbizwa hospitalini baada ya kujeruhiwa katika mashambulizi hayo.

Gavana wa jimbo la Homs, Talal Barazi, pia amesema sababu ya mashambulizi hayo bado haijulikani, ingawa amekiri kuwa ghala hilo linahifadhi silaha za jeshi, bila kueleza iwapo  linamilikiwa na kundi la Hezbollah au la.

Mashambulizi hayo ya leo Ijumaa yametokea katika jimbo la Homs, kati kati mwa Syria ambako pia kunapatikana vituo vya jeshi la taifa hilo.

Mashambulizi yalilenga ghala la silaha za jeshi

Libanon Ballbeck HisbollahParade
Wapiganaji wa Hezbollah wakishiriki gwaridePicha: Getty Images/AFP

Hata hivyo, Israel haijatoa tamko lolote kuhusiana  na  mashambulizi hayo. Israel imekuwa ikifanya mashambulizi ya mara kwa mara, la hivi karibuni likitokea Jumatatu kuyalenga maeneo ya makundi yenye mafungamano na Iran nchini Syria, huku ikisema kamwe haitoikubali Iran kuwa na ushawishi katika mataifa yanaopakana na Israel.

Mnamo Alhamisi Aprili 30.04.2020  shirika la habari la Syria liliripoti kuwa mashambulizi ya helikopta za Israel kutokea eneo la milima ya Golan yalisabadbisha uhabirifu mkubwa wa vifaa vya Syria.

Inafahamika kuwa ghala hilo lilikuwa na zana za kijeshi linamilikiwa na kundi la Hezbollah linaoungwa mkono na Iran, ambalo pia limekuwa likivisaidia vikosi vya Syria katika vita vya miaka tisa.

Katika miezi za hivi karibuni, maafisa wa Israel wameelezea wasi wasi wao kwamba kundi la Hezbollah liko katika harakati  za kuanzisha utengenezaji wa makombora nchini Syria.

Hata hiyvo serikali ya Syria imekanusha madai hayo, na kukana kwamba haina maghala yoyote ya  makundi yenye mfungamano na Iran.

Vyanzo: APE/DPAE