1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yaidhinisha vifaru vya Leopard kwa Ukraine

Amina Mjahid
25 Januari 2023

Ujerumani imeridhia kupelekwa nchini Ukraine vifaru vyake vya kivita aina ya Leopard 2 na kuidhinisha pia nchi washirika kama Poland, Uhispania, Finland, Uholanzi na Norway kuipatia Ukraine zana hizo za kijeshi.

https://p.dw.com/p/4Mh24
Bundeskanzler Olaf Scholz beim Kampfpanzer Leopard 2 A6 der Bundeswehr
Picha: Björn Trotzki/IMAGO

Msemaji wa serikali ya Ujerumani Steffen Hebe-streit amesema hatua ya kwanza itakayochukuliwa ni kutoa vifaru hivyo 14 kutoka katika hifadhi yake ya kijeshi.

Akiizungumzia hoja hiyo hii leo bungeni Kansela wa Ujerumani  Olaf Scholz amesema kando na kutoa vifaru hivyo Ujerumani itatoa mafunzo pia kwa wanajeshi wa Ukraine.

Scholz amesema nchi yake mara zote itakuwa mstari wa mbele linapokuja  suala la kuiunga mkono Ukraine. Poland na Uingereza, ambazo zimeahidi mizinga 14 kila moja, zimekaribisha uamuzi huo.

Uholanzi, Finland na Uhispania zimesema pia zilikuwa tayari kupeleka vifaru hivyo. Ukraine imeishukuru Ujerumani kwa hatua hiyo, huku Urusi ikilaani na kusema Ujerumani imetelekeza wajibu wake kwa Moscow.