1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mfalme Charles III kulihutubia bunge la Ujerumani

Bruce Amani
30 Machi 2023

Mfalme Charles III Uingereza atalihutubia bunge la Ujerumani na kuwa mfalme wa kwanza kufanya hivyo, katika ziara yake ya kwanza nje ya nchi akiwa mfalme.

https://p.dw.com/p/4PUTD
König Charles trifft Olaf Scholz
Picha: Matthias Schrader/AP/picture alliance

Ziara hiyo ya siku tatu nchini Ujerumani ni yake ya kwanza ya kigeni tangu alipokalia kiti cha Ufalme, na inatafsiriwa kama "ishara yenye nguvu" ya kujenga mahusiano ya baada ya Brexit na bara la Ulaya.

Mfalme Charles wa III awali alikutana na Kansela Olaf Scholz kabla ya kuelekea bungeni.

Mfalme wa Uingereza Charles lll aanza ziara ya kiserikali nchini Ujerumani

Akizungumza jana katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na mwenyeji wake Rais Frank-Walter Steinmeier, Charles alifisia kile alichokiita "thamani ya kudumu ya uhusiano wa Uingereza na Ujerumani."

Alisema uungaji mkono wa pamoja wa nchi hizo mbili kwa Ukraine katika vita vyake dhidi ya uchokozi usio na uchochezi wa Urusi unadhihirisha nia yao ya kulinda na kukuza maadili yao ya pamoja ya kidemokrasia.