1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBrazil

Jair Bolsonaro arejea Brazil kuuongoza upinzani

Zainab Aziz
30 Machi 2023

Rais wa zamani wa Brazil Jair Bolsonaro amerejea nchini baada ya kukaa nje ya nchi kwa muda wa miezi mitatu. Kiongozi huyo wa zamani wa Brazil alikuwa anaishi Florida, Marekani.

https://p.dw.com/p/4PVTN
USA, National Harbor | Jair Bolsonaro auf der CPAC
Picha: Roberto Schmidt/AFP/Getty Images

Bolsonaro alikaribishwa na mamnia ya wafuasi wake kwenye uwanja wa ndege wa Brasilia siku ya Alhamisi huku kukiwa na ulinzi mkali. Kwa mujibu wa maafisa wa chama chake cha Partido Liberal (PL) wamesema Rais huyo wa zamani wa Brazil Jair Bolsonaro, ambaye hakuwahi kukubali kushindwa kwenye uchaguzi wa mwaka jana ataongoza upande wa upinzani dhidi ya Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva.

Wafuasi wa Jair Bolsonaro walipomsubiri kuwasili nchini Brazil
Wafuasi wa Jair Bolsonaro walipomsubiri kuwasili nchini BrazilPicha: AFP

Bolsonaro aliondoka Brazil muda mfupi kabla ya muhula wake madarakani kukamilika. Hatua hiyo ilikiuka desturi na kuonesha kuwa kwa makusudi alikataa kukabidhi uongozi kwa mrithi wake, Luiz Inacio Lula da Silva, ambaye alishinda uchaguzi uliofanyika mwezi Oktoba mwaka uliopita wa 2022.

Akiwa nchini Marekani, Bolsonaro mara nyingi alijiepusha kutoa matamko hadharani ingawa alitoa hotuba kadhaa kwa wataalamu wa Brazil na wahafidhina ikiwa ni pamoja na katika Mkutano wa Kihafidhina wa katika jiji la Maryland.

Jair Bolsonaro akihutubia kwenye mkutano wa CPAC jijini Maryland tarehe 4.03.2023
Jair Bolsonaro akihutubia kwenye mkutano wa CPAC jijini Maryland tarehe 4.03.2023Picha: Roberto Schmidt/AFP/Getty Images

Hata hivyo makusudio ya Bolsonaro ya kurudisha umaarufu wake wa kisiasa yanaweza kukwama kutokana na kukabiliwa na mfululizo wa uchunguzi dhidi yake, ikiwa ni pamoja na kuchunguzwa iwapo alichochea uasi wa Januari 8.

Soma:Polisi wachunguza vito vya thamani vya Bolsonaro vilivyoingizwa Brazil

Hivi majuzi gazeti la Estado de S.Paulo lilifichua kuhusu masanduku matatu yaliyojaa vito vya gharama kubwa yanayodaiwa kuletwa kwa Bolsonaro kutoka Saudi Arabia hali ambayo inamuweka hatarini rais huyo wa zamani kufuatwa na mkondo wa sheria.

Steve Bannon, mshirika wa muda mrefu warais wa zamani wa Marekani Donakd Trump ameliambia gazeti la Brazil, Folha de S.Paulo kwamba Bolsonaro kamwe hakupaswa kuondoka nchini, na kwamba hakuna umuhimu wa kuchumchunguza kiongozi huyo.

Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva
Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da SilvaPicha: Eraldo Peres/AP Photo/picture alliance

Mbali na uchunguzi kuhusu vito vya almasi, Bolsonaro anakabiliwa na takriban tuhuma kumi na mbili zilizowasilishwa na mahakama zinazohusiana na matendo yake wakati wa kampeni za uchaguzi za mwaka jana hasa kuhusiana na madai yake ambayo hajayathibitishwa kuwa mfumo wa kielektroniki wa kupiga kura ulikuwa wa udanganyifu.

Ikiwa Bolsonaro atapatikana na hatia katika yoyote kati ya kesi hizo anaweza kupoteza haki zake za kisiasa na kuzuiwa kugombea urais katika uchaguzi ujao.

Vyanzo:AFP/AP/RTRE